KOCHA mpya wa klabu za TMK United, Kennedy Mwaisabula amekipangua kikosi chote cha timu hiyo aliyoirithi toka kwa Fred Felix Minziro na kuanza mipango ya kuisuka upya kwa ajili ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara itakayofanyika Septemba mwaka huu.
Akizungumza na Full Mswano, Mwaisabula aliyewahi kuzinoa timu za Yanga, Bandari-Mtwara na Twiga Sports, alisema ameamua kukifumua kikosi hicho kwa lengo la kuhakikisha TMK Utd inapanda Ligi Kuu msimu wa 2011-2012.
Mwaisabula alisema ameweza kubaini kuwa katika kikosi kilichoshindwa kufuzu ligi kuu msimu huu kilikuwa kimejaa wachezaji wengi wazee na waliocheza kwa muda mrefu ligi kuu na hivyo kukosa mbinu za kiuchezaji.
"Nakipangua kikosi baada ya kubaini waliokuwepo kwa sasa wengi wana umri mkubwa au kucheza kwa muda mrefu kwenye ligi na hivyo nitatafuta chipukizi ambao naamini watanisaidia na kuitumikia TMK kwa muda mrefu," alisema Mwaisabula.
Mwaisabula, alisema kutokana na mipango yake ya kuunda kikosi kipya, amewaalika wachezaji vijana na wenye uwezo wa kisoka kujitokeza kufanyiwa majaribio kwenye mazoezi ya timu hiyo yaliyoanza tangu siku ya Jumanne kwenye viwanja vya Sigara, Chang'ombe.
Mwaisabula alisema mbali na kuwaomba wachezaji chipukizi kujitokea uwanja wa TCC, pia mwenyewe atakuwa akiifuatilia michuano ya Copa Coca Cola kusaka wengine.
Baadhi ya wachezaji walioichezea TMK msimu uliopita na kuzidiwa ujanja na timu za Ruvu Shooting Stars, Kelvin Mhagama na wakali wengine waliowahi kzuichezea Simba na Yanga.
Tuesday, July 6, 2010
Snake Boy, Maugo kuzidunda PTA

PAMBANO litakalomrudisha tena ulingoni bingwa wa zamani wa ngumi za kulipwa nchini na
Duniani, Rashid Matumla 'Snake Boy' dhidi ya Mada Maugo litarajiwa kupigwa kwenye ukumbi
wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Rais wa Organaizesheni ya Ngumi za Kulipwa nchini, TPBO, Yasin Abdallah
'Ustaadh', pambano hilo lisilo la kuwania mkanda wowote litafanyika Julai 18 mwaka huu.
Rais huyo alisema pambano hilo la raundi nane, limepangwa kufanyika kwenye ukumbi huo wa
PTA kutokana na kuwezesha mashabiki wa ngumi jijini kuweza kulishuhudia kwa raha zao
sambamba na michezo mingine ya utangulizi itakayolisindikiza pigano hilo maalum.
"Lile pambano linalosubiriwa kwa hamu kati ya Snake Boy na Maugo litafanyika kwenye ukumbi
wa PTA na maandalizi kwa ujumla yanaendelea vema, ikiwemo kuthibitisha kwa mabondia
watakaopamba ulingoni kulisindikiza siku hiyo ya Julai 18," alisema Ustaadh.
Ustaadh, alisema mpambano huo umeandaliwa maalum kwa nia ya kumaliza ubishi baina ya
mabondia hao wawili ambao wamekuwa wakitambia kwa muda mrefu.
"Pamoja na lengo la kukuza na kuendeleza mchezo wa ngumi, lakini pia kubwa ni kumaliza ubishi
baina ya mabondia hao wawili ambao wamekuwa wakitambiana kila kukicha, kila mmoja
akitamba ni mkali zaidi ya mwenzake," alisema.
Alisema pambano hilo la uzito wa kilo 72, limeanza kuamsha hisia za wapenzi na mashabiki wa
ngumi wanaotaka kujua nani zaidi baina ya mabondia hao wawili.
Ustaadh aliwaomba wadau mbalimbali wa mchezo wa ngumi kujitokeza kulidhamini pambano
hilo kwa nia ya kurejesha nguvu na hamasa katika mchezo huo wa ngumi.
"Wakati mabondia wakiendelea kujifua kwa ajili ya kuonyeshana umwamba ulingoni, tulikuwa
tunawaomba wadau na watu mbalimbali kujitokeza kulidhamini pambano hilo, ili kuongeza
hamasa na ushindani baina yao," alisema.
Mhazini Simba 'awekwa' kiporo
UONGOZI wa klabu ya soka ya Simba umeshindwa kumtangaza Mhazini Mkuu wa klabu hiyo
kama ulivyokuwa umeahidi kwa maelezo kwamba hata akiteuliwa hatakuwa na kazi za kufanya
kwa sasa.
Hata hivyo uongozi huo umesisitiza kuwa muda muafaka ukifika mtu wa kushika nafasi hiyo
atateuliwa kuungana na Afisa Utawala na Msemaji wa klabu ambao tayari wameshaanza kazi
ndani ya klabu hiyo.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage, alisema kamati yao ya utendaji imeona ni vema kuachana na
uteuzi wa mhazini mkuu kwa sasa kwa vile majukumu mengi ndani ya klabu yao yapo kwa Afisa
Utawala anayekaimu pia Ukatibu Mkuu na msemaji mkuu walioteuliwa hivi karibuni.
Rage, alisema hata kama watamteua hivi sasa mhazini hatakuwa na kazi za kufanya kama ilivyo
kwa Evodius Mtawala ambaye ni Afisa Utawala au Cliford Ndimbo aliyerejeshewa cheo chake cha usemaji mapema wiki hii.
"Ni kweli tulikuwa na nia ya kuteua mhazini mkuu, lakini tumeona wawili hawa wa kwanza ndio
muhimu na wanaohitajika haraka na muda ukifika wa kumtaka Mhazini tutamteua," alisema Rage.
Rage aliongeza kuwa, kama alivyoahidi akiingia madarakani ni kwamba ndani ya siku zake 100
zitakazokamilika Agosti 17, ikiwa ni siku nne kabla ya kuanza kwa ligi kuu msimu huu, kila kitu
kitakuwa kimeenda sawa na hivyo wanachama wa Simba hawapaswi kuwa na shaka nae.
"Wenyewe wanaona mambo yanavyoenda vema, jengo sasa linakarabatiwa, tayari tuna afisa
utawala na msemaji, uwanja wa mazoezi upo na bado kuna mengine yanakuja kabla hata zile siku
100 hazijakamilika," alisema Rage.
Rage aliwaomba wanachama wa Simba wakati akiingia madarakani Mei 9 kuwa wampe siku 100
kuweza kuibadilisha klabu yao toka katika hali mbaya iliyokuwa nayo hadi kurejea enzi zake na
moja ya vitu alivyotilia mkazo ni kuimarisha uongozi na kulikarabati jengo vituo vilivyofanyika.
Nagy Kaboyoka: Atangaza kumvaa Anne Kilango
MWENYEWE anasema mwaka 2005 kura 'hazikutosha', ndio maana hakuweza kuteuliwa kuwa mgombea wa Ubunge Jimbo la Same Mashariki kupitia chama tawala, CCM.
Hata hivyo, anasema katika uchaguzi mkuu ujao ambao mbio zake zimeanza rasmi ndani ya chama hicho, ana imani kubwa ya kura zake kutosha na kupitishwa kuipigania CCM katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini nzima Oktoba mwaka huu.
Majina yake kamili ni Naghenjwa 'Nagy' Livingstone Kaboyoka, mwanaharakati wa maendeleo ya jamii, mmoja wa wagombea waliotangaza nia ya kutaka kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Same Mashiriki ambalo kwa sasa kinashikiliwa na Anne Kilango Maceleca.
Mwanamama huyo mwenye shahada ya pili na masuala ya Maendeleo ya Jamii aliyoipata nchini Uingereza na mtaalam wa lugha mbalimbali za kimataifa, alisema ana imani uchaguzi mkuu wa mwaka huu atapata fursa kuiwakilisha CCM na kushinda kiti cha jimbo hilo.
Alisema kitu kinachompa jeuri ya kuamini kuwa ataibuka ushindi ni utaratibu mpya wa mfumo wa upigaji kura ndani ya CCM katika uteuzi wa wagombea wa chama hicho, pia uungwaji mkono aliopata toka kwa wakazi wa jimbo hilo tangu ulipomalizika uchaguzi wa mwaka 2005.
"Pamoja na kutambua upinzani utakuwa mkubwa ndani ya CCM, lakini taratibu na kanuni mpya zinazojumuisha wingi wa wapiga kura kura tofauti na zamani ilipokuwa kikundi kidogo tu cha watu ndicho kinachonipa nguvu ya kushinda," alisema Nagy.
Alisema pamoja na kwamba tayari wanachama wenzake kadhaa wameshajitokeza kutaka kuwania kiti hicho hicho akiwemo mtetezi, Anne Kilango, hana hofu yoyote kwa vile anajiamini uzoefu wake katika kujitolea katika huduma za maendeleo ya jamii ni silaha kubwa kwake.
Mwanamama huyo aliyeolewa na mwenye watoto watatu, alisema yeye ni mwenyeji wa jimbo hilo na kipindi cha nyuma kabla ya kwenda nje ya nchi kulitumikia taifa lake, alisaidia mno kuanzishwa miradi mbalimbali ya kijamii ambayo iliwasaidia wakazi wa jimbo hilo.
Alisema kutokana na hilo na dhamira yake ya kweli ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Jimbo hilo waliokata tamaa ya kimaisha kutokana na umaskini mkubwa walionao licha ya kuwa katika jimbo lenye utajiri wa rasilimali, anaamini hakuna wa kumdondosha.
Nagy, aliyewahi kufanya kazi Ubalozi wa Tanzania nchini Denmark, alisema kikubwa atakachozingatia iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo, ni kuwashirikisha wananchi katyika kujiletea maendeleo ili kuondoka na hali ya umaskini walionao.
"Nimeamua kujitokeza kuwania Ubunge wa Jimbo la Same Mashariki, kubwa ni kuhakikisha
rasilimali zilizopo jimboni humo ziweze kuwainua wananchi kiuchumi kwa kuwashirikisha katika miradi kutokana na kubobea katika shughuli za maendeleo ya jamii," alisema.
Aliongeza kuwa, anaamini rasilimali zilizopo katika jimbo hilo zikitumiwa vema kwa kuwashirikisha wananchi zinaweza kuwaondolea umaskini na kuwaletea maendeleo yanayoweza kulinganishwa na majimbo mengine ya wilaya yao ya Same ambayo yapo juu kwa sasa.
Alisema mbali na kuwashirikisha wananchi katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo na uchumi, lakini pia ataelekeza nguvu zake katika kuboresha mazingira na huduma za kijamii ili kuwafanya wakazi wa jimbo hilo kuifaidi 'keki' ya Uhuru wa Tanzania.
"Ni aibu kwa mkulima wa jimbo hili lenye rasilimali nyingi kutembea karibu kilomita 10 kwa miguu kupeleka mazao yake sokoni, sisemi kama hakuna kilichofanyika, ila kunahitajika mtu wa kuleta mabadiliko ya kweli na sio kupiga kelele tu," alisema Nagy, Afisa Utumishi wa Hospitali ya Kinondoni.
Kuhusu vita dhidi ya ufisadi, alisema haipaswi kufanywa kwa makelele bila utekelezaji wa vitendo ili kukomesha matendo hayo na kuwasaidia wananchi kuinua kimaendeleo na uchumi.
"Kelele zinazopigwa kama hazileti tija na ufanisi wa kweli, wananchi wanaweza wasiwaelewe wanaovipigana kwa sababu hawaoni mabadiliko katika maisha yao ya kila siku, hivyo ni vema tushikamane na kuupiga vita ufisadi kikwelikweli na sio kupiga blabla tu," alisema Nagy.
Alipoulizwa haoni kama atapata upinzani mkubwa kutokana na watu waliojitokeza hadi sasa katika kuwania jimbo hilo akiwemo anayekishikilia kiti hicho, Nagy alisema hahofii mtu yeyote kwa vile anajiamini ana uwezo wa kushinda na kuwaongoza wakazi wa jimbo hilo.
"Pamoja na kufahamu changamoto zilizopo, lakini safari hii nimejipanga vema na simuhofii yeyote kwa sababu mahakimu wetu ni wananchi ambao ndio walionisihi kugombea tangu mwaka 2005, ingawa nilikwamishwa katika kura za maoni na kwa utaratibu wa sasa naamini nitashinda," alisema.
Mwanamama huyo alizaliwa Agosti 8, 1949 na amesoma hadi kufikia ngazi ya Chuo Kikuu na amewahi kufanya kazi sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi, akijishughulisha na masuala ya maendeleo ya kijamii, kama miradi ya maji, afya na mengineyo.
Hata hivyo, anasema katika uchaguzi mkuu ujao ambao mbio zake zimeanza rasmi ndani ya chama hicho, ana imani kubwa ya kura zake kutosha na kupitishwa kuipigania CCM katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini nzima Oktoba mwaka huu.
Majina yake kamili ni Naghenjwa 'Nagy' Livingstone Kaboyoka, mwanaharakati wa maendeleo ya jamii, mmoja wa wagombea waliotangaza nia ya kutaka kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Same Mashiriki ambalo kwa sasa kinashikiliwa na Anne Kilango Maceleca.
Mwanamama huyo mwenye shahada ya pili na masuala ya Maendeleo ya Jamii aliyoipata nchini Uingereza na mtaalam wa lugha mbalimbali za kimataifa, alisema ana imani uchaguzi mkuu wa mwaka huu atapata fursa kuiwakilisha CCM na kushinda kiti cha jimbo hilo.
Alisema kitu kinachompa jeuri ya kuamini kuwa ataibuka ushindi ni utaratibu mpya wa mfumo wa upigaji kura ndani ya CCM katika uteuzi wa wagombea wa chama hicho, pia uungwaji mkono aliopata toka kwa wakazi wa jimbo hilo tangu ulipomalizika uchaguzi wa mwaka 2005.
"Pamoja na kutambua upinzani utakuwa mkubwa ndani ya CCM, lakini taratibu na kanuni mpya zinazojumuisha wingi wa wapiga kura kura tofauti na zamani ilipokuwa kikundi kidogo tu cha watu ndicho kinachonipa nguvu ya kushinda," alisema Nagy.
Alisema pamoja na kwamba tayari wanachama wenzake kadhaa wameshajitokeza kutaka kuwania kiti hicho hicho akiwemo mtetezi, Anne Kilango, hana hofu yoyote kwa vile anajiamini uzoefu wake katika kujitolea katika huduma za maendeleo ya jamii ni silaha kubwa kwake.
Mwanamama huyo aliyeolewa na mwenye watoto watatu, alisema yeye ni mwenyeji wa jimbo hilo na kipindi cha nyuma kabla ya kwenda nje ya nchi kulitumikia taifa lake, alisaidia mno kuanzishwa miradi mbalimbali ya kijamii ambayo iliwasaidia wakazi wa jimbo hilo.
Alisema kutokana na hilo na dhamira yake ya kweli ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Jimbo hilo waliokata tamaa ya kimaisha kutokana na umaskini mkubwa walionao licha ya kuwa katika jimbo lenye utajiri wa rasilimali, anaamini hakuna wa kumdondosha.
Nagy, aliyewahi kufanya kazi Ubalozi wa Tanzania nchini Denmark, alisema kikubwa atakachozingatia iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo, ni kuwashirikisha wananchi katyika kujiletea maendeleo ili kuondoka na hali ya umaskini walionao.
"Nimeamua kujitokeza kuwania Ubunge wa Jimbo la Same Mashariki, kubwa ni kuhakikisha
rasilimali zilizopo jimboni humo ziweze kuwainua wananchi kiuchumi kwa kuwashirikisha katika miradi kutokana na kubobea katika shughuli za maendeleo ya jamii," alisema.
Aliongeza kuwa, anaamini rasilimali zilizopo katika jimbo hilo zikitumiwa vema kwa kuwashirikisha wananchi zinaweza kuwaondolea umaskini na kuwaletea maendeleo yanayoweza kulinganishwa na majimbo mengine ya wilaya yao ya Same ambayo yapo juu kwa sasa.
Alisema mbali na kuwashirikisha wananchi katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo na uchumi, lakini pia ataelekeza nguvu zake katika kuboresha mazingira na huduma za kijamii ili kuwafanya wakazi wa jimbo hilo kuifaidi 'keki' ya Uhuru wa Tanzania.
"Ni aibu kwa mkulima wa jimbo hili lenye rasilimali nyingi kutembea karibu kilomita 10 kwa miguu kupeleka mazao yake sokoni, sisemi kama hakuna kilichofanyika, ila kunahitajika mtu wa kuleta mabadiliko ya kweli na sio kupiga kelele tu," alisema Nagy, Afisa Utumishi wa Hospitali ya Kinondoni.
Kuhusu vita dhidi ya ufisadi, alisema haipaswi kufanywa kwa makelele bila utekelezaji wa vitendo ili kukomesha matendo hayo na kuwasaidia wananchi kuinua kimaendeleo na uchumi.
"Kelele zinazopigwa kama hazileti tija na ufanisi wa kweli, wananchi wanaweza wasiwaelewe wanaovipigana kwa sababu hawaoni mabadiliko katika maisha yao ya kila siku, hivyo ni vema tushikamane na kuupiga vita ufisadi kikwelikweli na sio kupiga blabla tu," alisema Nagy.
Alipoulizwa haoni kama atapata upinzani mkubwa kutokana na watu waliojitokeza hadi sasa katika kuwania jimbo hilo akiwemo anayekishikilia kiti hicho, Nagy alisema hahofii mtu yeyote kwa vile anajiamini ana uwezo wa kushinda na kuwaongoza wakazi wa jimbo hilo.
"Pamoja na kufahamu changamoto zilizopo, lakini safari hii nimejipanga vema na simuhofii yeyote kwa sababu mahakimu wetu ni wananchi ambao ndio walionisihi kugombea tangu mwaka 2005, ingawa nilikwamishwa katika kura za maoni na kwa utaratibu wa sasa naamini nitashinda," alisema.
Mwanamama huyo alizaliwa Agosti 8, 1949 na amesoma hadi kufikia ngazi ya Chuo Kikuu na amewahi kufanya kazi sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi, akijishughulisha na masuala ya maendeleo ya kijamii, kama miradi ya maji, afya na mengineyo.
Vita ya Uholanzi na Uruguay ni kesho * Ni katika mechi ya nusu fainali ya WOZA 2010, Ujerumani, Spain kumalizana J'5

CAPE TOWN, Afrika Kusini

BAADA ya kufanikiwa kuzing'oa 'kimiujiza' timu za Brazil na Ghana katika hatua ya robo fainali, Uholanzi na Uruguay usiku wa kesho zinatarajiwa kuonyeshana kazi kwenye pambano la Nusu Fainali ya kwanza ya michuano ya Fainali za Kombe la Dunia 2010 zinazofanyika nchini hapa.
Pambano hilo litakalochezwa kwenye dimba la Green Point, uliopo Cape Town, linatajaliwa kuwa kali kutokana na soka la lililoonyeshwa na timu zote katika mechi za michuano ya mwaka huu.
Uholanzi inayofahamika kama 'The Orange' wanakutana na Uruguay baada ya kuisambaratisha Brazil kwa kipigo cha mabao 2-1 na kufikia rekodi yao ya kucheza hatua hiyo kwa mara ya nne baada ya kufanya hivyo fainali za mwaka 1974, 1978 na 1998.
Ikiwa na wachezaji wenye vipaji na uwezo mkubwa wa kusukuma gozi kama Robin Van Perse, Arjen Robben, Wesley Sneijder, Nigel de Jong, Mark van Bommel, Giovanni van Bronckhorst, Dirk Kuyt na wengineo leo itakuwa na kazi kubwa kuweza kuizuia Uruguay iliyoing'oa Ghana.
Kama ilivyo kwa Uruguay, ambayo haijaonja kipigo chochote katika michuano ya WOZA 2010, Uholanzi itataka kushinda mechi hiyo na kufuzu fainali ikirejea mafanikio ya fainali mbili mfululizo za mwaka 1974 na 1978, iliyoishia kulikosa kombe kwa Ujerumani na Argentina.
Pengine mwaka huu Uholanzi itapenda sio kufuzu fainali tu bali kuvunja mwisho wa kutotwaa taji hilo licha ya kuwa nchi yenye wachezaji wenye uwezo miubwa kisoka duniani.
Hata hivyo itawabidi Uholanzi wafanye kazi ya ziada mbele ya Uruguay ilifuzu hatua hiyo ya fainali ikiwa ni baada ya miaka 40, kwa kuing'oa wawakilishi wa Afrika, Ghana kwa mikwaju ya penati 4-2 kufuatia kumaliza dakika 120 zikitoka sare ya bao 1-1.
Uruguay yenye mshambuliaji mwenye njaa ya magoli, Diego Forlan, Luis Suarez, Alvaro Pereira, Diego Perez na wengine bila shaka haitakubali kirahisi kuwa ngazi ya kuwafusha wapinzani wao fainali wakati wenyewe wanapenda kufika huko kurejea kurejea mafanikio ya fainali za 1930 na 1950 waliibuka mabingwa wa fainali hizo.
Hivyo pambano hilo la kesho ni gumu kutabirika kutokana na rekodi za timu zote mbili ambazo kila mmoja inampa nafasi sawa ya kuibuka na ushindi na kutinga fainali kusubiri kucheza na mshindi wa mechi nyingine ya hatua hiyo inayochezwa Jumatano kati ya Ujerumani na Spain.
Ujerumani ilipata nafasi hiyo baada ya kuisasambua Argentina kwa mabao 4-0, huku Spain ikipata ushindi 'kiduchu' wa bao 1-0 dhidi ya Paraguay.
Mechi ya fainali za WOZA 2010 itachezwa siku ya Jumapili kwenye dimba la Soccer City, Johannesburg.
Wanamuziki zaidi ya 200 wafa nchini
TANZANIA imefiwa na wanamuziki zaidi ya 200 waliofariki kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo magonjwa na ajali.
Takwimu hizi hazijatolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wala Chama cha muziki
wa Dansi nchini CHAMUDATA, bali mwanamuziki mkongwe nchini, Yusuph Subwa.
Mwanamuziki huyo ambaye amewahi kuzipigia bendi mbalimbali nchini zikiwemo Afro 70 ya
marehemu Patrick Balisidya na Super Matimila ya Dr Remmy Ongala, amesema kuwa yeye
mwenyewe amewahesabu na tayari wamefika 200.
Subwa ambaye kwa sasa analiongoza kundi la Exel 1 lenye makao makuu yake Temeke Sokota,
ametunga kibao cha kuwakumbuka marehemu wote ambao ni wanamuziki.
"Katika hicho kibao nimewataja wanamuziki wote waliofariki nchini tangu enzi hizo, katika
karatasi yangu nina wanamuziki 200 hao wa Kitanzania tu waliofariki na wote ninawataja kwenye nyimbo yangu," alisema.
Amesema kuwa hapo hajataja wanamuziki wa Kikongomani ambao walikuwa na bendi mbalimbali nchini ambao wamefariki dunia na kuzikwa hapa hapa nchini.
"Mimi hao sikuwataja, ila nimewataja Watanzania tu ambao kusema kwei waliipaisha nchi yetu
kwenye ramani ya muziki nchi za nje, amini usiamini wako 200 na kama nikiendelea kuwakumbuka waongezeka kidogo," alisema.
Subwa ambaye ni mpiga drums, amesema kuwa katika historia ya maisha yake wamesafiri nchi
mbalimbali za nje hasa bara la Ulaya akiwa bendi ya Super Matimila ambapopia katika ziara yao
wameshawahi kupiga jukwaa moja na hayati Franco wa Kongo na Manu Dibango wa Cameroon
na kupata wasaa wa kubadilishana nao mawazo wakiwa pamoja na Remmy aliyeokoa kwa sasa.
Mr Ebbo asita kuingiza albamu sokoni, kisa...!

Mr. Ebbo asita kuweka albamu sokoni
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, 'Mr.Ebbo' amesema amesita kuingiza sokoni albamu yake
mpya ambayo hajaipa jina kwa madai albamu ya sita bado inaendelea kufanya vema kwa sasa.
Mr. Ebbo ambaye jina lake halisi ni Abel Loshilaa Motika, aliiambia Blog hii kwa njia ya simu toka
Tanga kuwa albamu yake ya sita iitwayo 'Watoto Wangu' bado ina mashabiki wengi.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo, imeona ni vyema kuisitisha kwanza albamu ya saba ambayo
nayo amesema nyimbo zake zimakamilika na zimesharekodiwa katika studio yake ya Motika
Records.
"Nina albamu ya saba yenye nyimbo za Uzuri wa Kichina, Mama Rosa, Ninasaini, na Wazazi
Wangu ambazo kwa kweli ni moto wa kuotea mbali, lakini siipeleki sokoni kwa sasa," alisema Mr.
Ebbo.
Alisema kuwa nyimbo za albamu ya sita zinazoendelea kutesa sokoni ni 'Hajui Kupika',
'Kahamishwa', 'Kaka Hoza', 'Maisha Plastiki', 'Kunanuna', 'Mbado remix', 'Sikopi Tena', na 'Ulimi'.
Msanii huyo aliendelea kutaja nyimbo nyingine za albamu hiyo kuwa ni 'Bodaboda', 'Simu Feki',
'Tabia Mbaya' na 'Bado Naimba' ambazo alisema ameziachia nafasi ili ziendelee kumtangaza.
Mr. Ebbo aliyeibuka kwenye muziki wa kizazi kipya mwaka 2002, aliwahi kutamba na albamu yake
ya kwanza ya 'Fahari Yako' na nyingine kama 'Bado Ijasungumiswa', 'Kazi Gani', 'Alibamu',
'Kamongo' na ndipo alipoachia hiyo ya 'Watoto Wangu' inayoendelea kutamba sokoni.
Subscribe to:
Comments (Atom)