Friday, December 9, 2011

Mourinho ‘auchuna’ Real wakiivaa Barca



MADRID, Hispania
KOCHA Jose Mourinho wa Real Madrid aliamua kutozungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa kawaida wa kabla ya mechi jana na msaidizi wake, Aitor Karanka, ndiye aliyetarajiwa kujibu maswali badala yake kuhusiana na mechi yao ya kwanza ya ‘Clasico’ watakayocheza nyumbani leo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Barcelona, Real walisema kupitia tovuti yao (www.realmadrid.com).
Mourinho amekuwa na mahusiano mabaya na vyombo vya habari vya jiji la Madrid tangu alipotua akitokea Inter Milan mwishoni mwa msimu wa 2009-10 na alikataa kuzungumza kabla ya mechi yao ya La Liga dhidi ya Barca April na kusababaisha waandishi wa habari takribani 30 kuamua kutoka nje ya ukumbi. Kocha wa Barca, Pep Guardiola alitarajiwa kuzungumza na waandishi baadaye jana.
Huku takriban theluthi ya mechi za msimu zikiwa tayari zimeshachezwa, vinara Real wanaongoza kwa tofauti ya pointi tatu na pia wana mechi moja mkononi kulinganisha na Barca wanaowafuatia katika nafasi ya pili kwenye msimamo, ambao wanafukuzia rekodi ya klabu yao ya kutwaa ubingwa wa La Liga kwa mara ya nne mfululizo.
Real wameshinda katika mechi zao 10 zilizopita za La Liga, na mechi 15 mfululizo za michuano yote hadi sasa, wakati Barca wamefungwa katika mechi moja tu kati ya 11 za 'Clasicos' dhidi ya mahasimu wao wa jadi tangu Guardiola atwae madaraka mwaka 2008.
Kiungo huyo wa zamani wa Barca na timu ya taifa ya Hispania hajawahi kufungwa kwenye Uwanja wa Bernabeu akiwa kocha, akishinda mechi tatu na kupata sare mbili huku kikosi chake kikifunga mabao 13 na kuruhusu matano tu
Mourinho ana wakali wake wote kikosini isipokuwa beki wa kati wa kimataifa kutoka Ureno, Ricardo Carvalho, ambaye bado anauguza jeraha la goti na hajacheza tangu mwishoni mwa Septemba.
Guardiola pia ana wachezaji wake wote, ukiondoa Ibrahim Afellay, ambaye kwa muda mrefu sasa yuko nchini kwao Uholanzi akiuguza jeraha la goti alilofanyiwa upasuaji.

RATIBA YA LA LIGA (HISPANIA)
LEO, Jumamosi
Real Madrid v Barcelona (Saa 6:00) usiku
Levante v Sevilla (Saa 2:00) usiku
Betis v Valencia

RATIBA LIGI KUU ENGLAND
LEO Jumamosi
Arsenal v Everton (saa 12:00) jioni
Man U v Wolves (saa 12:00) jioni
Liverpool v QPR (saa 12:00) jioni
Bolton v Villa
Norwich v Newcastle
Swansea v Fulham
West Brom v Wigan

Kesho, Jumapili
Stoke v Tottenham (saa 1:00) usiku
Sunderland v Blackburn

KESHOKUTWA, Jumatatu
Chelsea v Man City (saa 5:00) usiku

No comments:

Post a Comment